5. Uniongoze katika ukweli wako na kunifundisha,kwani wewe ni Mungu, mwokozi wangu;ninakutegemea wewe kila siku.
6. Uikumbuke huruma yako ee Mwenyezi-Mungu;uzikumbuke na fadhili zako kuu,ambazo zimekuwako tangu kale.
7. Usikumbuke dhambi na makosa ya ujana wangu;unikumbuke kadiri ya fadhili zako,kwa ajili ya wema wako, ee Mwenyezi-Mungu.
8. Mwenyezi-Mungu ni mwema na mnyofu,kwa hiyo huwafundisha wenye dhambi njia.
9. Huwaongoza wanyenyekevu katika uadilifu;naam, huwafundisha hao njia yake.
10. Mwenyezi-Mungu hutenda kwa fadhili na uaminifu,kwa wale wanaoshika agano lake na maamuzi yake.
11. Kwa ajili ya jina lako, ee Mwenyezi-Mungu,unisamehe kosa langu kwani ni kubwa.
12. Kila mtu anayemcha Mwenyezi-Mungu,Mwenyezi-Mungu atamfunza njia ya kufuata.
13. Mtu wa namna hiyo atafanikiwa daima,na wazawa wake watamiliki nchi.
14. Mwenyezi-Mungu ni rafiki ya wale wamchao;yeye huwajulisha hao agano lake.
15. Namwangalia Mwenyezi-Mungu daima;yeye atainasua miguu yangu mtegoni.
16. Unielekee, ee Mungu, unionee huruma,maana mimi ni mpweke na mnyonge.