18. Uangalie mateso yangu na dhiki yangu;unisamehe dhambi zangu zote.
19. Angalia jinsi walivyo wengi maadui zangu;ona jinsi wanavyonichukia kwa ukatili.
20. Uyalinde maisha yangu, uniokoe;nakimbilia usalama kwako,usikubali niaibike.
21. Wema na uadilifu vinihifadhi,maana ninakutumainia wewe.
22. Ee Mungu, uwaokoe watu wako, Israeli;uwaokoe katika taabu zao zote.