Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 24:5-10 Biblia Habari Njema (BHN)

5. Mtu huyo atapokea baraka kwa Mwenyezi-Mungu,na haki yake kwa Mungu mwokozi wake.

6. Ndio hali ya kizazi cha watu wamtafutao yeye;naam, watu wamtafutao Mungu wa Yakobo.

7. Fungukeni enyi milango;fungukeni enyi milango ya kale,ili Mfalme mtukufu aingie.

8. Ni nani huyo Mfalme mtukufu?Ni Mwenyezi-Mungu, mwenye nguvu na uwezo;Mwenyezi-Mungu, mwenye uwezo vitani.

9. Fungukeni enyi malango,fungukeni enyi milango ya kale,ili Mfalme mtukufu aingie.

10. Ni nani huyo Mfalme mtukufu?Ni Mwenyezi-Mungu, wa majeshi,yeye ndiye Mfalme mtukufu.

Kusoma sura kamili Zaburi 24