18. Wanagawana nguo zangu,na kulipigia kura vazi langu.
19. Lakini wewe ee Mwenyezi-Mungu, usikae mbali nami;ewe msaada wangu, uje haraka kunisaidia.
20. Iokoe nafsi yangu mbali na upanga,yaokoe maisha yangu makuchani mwa mbwa hao!
21. Uniokoe kinywani mwa simba;iokoe nafsi yangu dhaifu toka pembe za nyati hao.
22. Nitawasimulia ndugu zangu matendo yako;nitakusifu kati ya kusanyiko lao:
23. Enyi mnaomcha Mwenyezi-Mungu, msifuni!Mtukuzeni enyi wazawa wote wa Yakobo!Mcheni Mungu enyi wazawa wote wa Israeli!
24. Maana yeye hapuuzi au kudharau unyonge wa mnyonge;wala hajifichi mbali naye,ila humsikia anapomwomba msaada.
25. Kwa sababu yako ninakusifukatika kusanyiko kubwa la watu;nitatimiza ahadi zangu mbele yao wakuchao.
26. Maskini watakula na kushiba;wanaomtafuta Mwenyezi-Mungu watamsifu.Mungu awajalie kuishi milele!
27. Ulimwengu wote utakumbuka na kumrudia Mwenyezi-Mungu;jamaa zote za mataifa zitamwabudu.
28. Maana Mwenyezi-Mungu ni mfalme;yeye anayatawala mataifa.