14. Nimekwisha kama maji yaliyomwagika;mifupa yangu yote imeteguka;moyo wangu ni kama nta,unayeyuka ndani mwangu.
15. Koo langu limekauka kama kigae;ulimi wangu wanata kinywani mwangu.Umeniacha kwenye mavumbi ya kifo.
16. Genge la waovu limenizunguka;wananizingira kama kundi la mbwa;wamenitoboa mikono na miguu.
17. Nimebaki mifupa mitupu;maadui zangu waniangalia na kunisimanga.
18. Wanagawana nguo zangu,na kulipigia kura vazi langu.
19. Lakini wewe ee Mwenyezi-Mungu, usikae mbali nami;ewe msaada wangu, uje haraka kunisaidia.
20. Iokoe nafsi yangu mbali na upanga,yaokoe maisha yangu makuchani mwa mbwa hao!
21. Uniokoe kinywani mwa simba;iokoe nafsi yangu dhaifu toka pembe za nyati hao.
22. Nitawasimulia ndugu zangu matendo yako;nitakusifu kati ya kusanyiko lao: