1. Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?Mbona uko mbali sana kunisaidia,mbali na maneno ya kilio changu?
2. Ee Mungu wangu, nalia mchana lakini hujibu;napiga yowe usiku, lakini nafuu sipati.
3. Hata hivyo, wewe ni mtakatifu;wewe watawala na kusifiwa na Waisraeli.
4. Wazee wetu walikutegemea;walikutegemea, nawe ukawaokoa.