Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 22:1-4 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?Mbona uko mbali sana kunisaidia,mbali na maneno ya kilio changu?

2. Ee Mungu wangu, nalia mchana lakini hujibu;napiga yowe usiku, lakini nafuu sipati.

3. Hata hivyo, wewe ni mtakatifu;wewe watawala na kusifiwa na Waisraeli.

4. Wazee wetu walikutegemea;walikutegemea, nawe ukawaokoa.

Kusoma sura kamili Zaburi 22