4. Mwenyezi-Mungu atawalaye juu mbinguni,anawacheka na kuwadhihaki.
5. Kisha, anawakaripia kwa ghadhabu,na kuwatisha kwa hasira, akisema:
6. “Nimemtawaza mfalme niliyemteua,anatawala Siyoni, mlima wangu mtakatifu!”
7. Mfalme asema: “Nitatangaza azimio la Mwenyezi-Mungu.Mungu aliniambia:‘Wewe ni mwanangu,mimi leo nimekuwa baba yako.
8. Niombe nami nitakupa mataifa yawe urithi wako,na dunia nzima kuwa mali yako.
9. Utawaponda kwa fimbo ya chuma;utawavunja kama chungu cha mfinyanzi!’”
10. Sasa enyi wafalme, tumieni busara;sikilizeni onyo hili, enyi watawala wa dunia.
11. Mtumikieni Mwenyezi-Mungu kwa uchaji;
12. msujudieni na kutetemeka;asije akakasirika, mkaangamia ghafla;kwani hasira yake huwaka haraka.Heri yao wote wanaokimbilia usalama kwake!