Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 2:1-8 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Kwa nini mataifa yanafanya ghasia?Mbona watu wanafanya njama za bure?

2. Wafalme wa dunia wanajitayarisha;watawala wanashauriana pamoja,dhidi ya Mwenyezi-Mungu na mteule wake.

3. Wanasema: “Tujiondoe katika utawala wao;tutupilie mbali minyororo yao!”

4. Mwenyezi-Mungu atawalaye juu mbinguni,anawacheka na kuwadhihaki.

5. Kisha, anawakaripia kwa ghadhabu,na kuwatisha kwa hasira, akisema:

6. “Nimemtawaza mfalme niliyemteua,anatawala Siyoni, mlima wangu mtakatifu!”

7. Mfalme asema: “Nitatangaza azimio la Mwenyezi-Mungu.Mungu aliniambia:‘Wewe ni mwanangu,mimi leo nimekuwa baba yako.

8. Niombe nami nitakupa mataifa yawe urithi wako,na dunia nzima kuwa mali yako.

Kusoma sura kamili Zaburi 2