Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 12:2-8 Biblia Habari Njema (BHN)

2. Kila mmoja humdanganya mwenzake,husema kwa kudanganya na kwa moyo wa unafiki.

3. Ee Mwenyezi-Munguuikomeshe hiyo midomo ya udanganyifu,na ndimi hizo zinazojigamba kupindukia.

4. Wao husema: “Kwa ndimi zetu tutashinda;midomo tunayo, nani awezaye kututawala?”

5. Lakini Mwenyezi-Mungu asema:“Kwa sababu maskini wanadhulumiwa,na wahitaji wanapiga kite, sasa naja,nami nitawapa usalama wanaoutazamia.”

6. Neno la Mwenyezi-Mungu ni safi,safi kama fedha iliyosafishwa katika tanuri,naam, kama fedha iliyosafishwa mara saba.

7. Utulinde, ee Mwenyezi-Mungu,utukinge daima na kizazi hiki kiovu.

8. Waovu wanazunguka kila mahali;upotovu unatukuzwa kati ya watu.

Kusoma sura kamili Zaburi 12