Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 10:7-17 Biblia Habari Njema (BHN)

7. Kinywa chake kimejaa laana, udanganyifu na dhuluma;mwepesi kusema maneno ya kuchukiza na maovu.

8. Hujificha vijijini huku anaotea,amuue kwa siri mtu asiye na hatia.Yuko macho kumvizia mnyonge;

9. huotea mafichoni mwake kama simba.Huvizia apate kuwakamata maskini;huwanasa kwa mtego wake na kuwachukua.

10. Mnyonge huvamiwa na kuangushwa chini;huangushwa kwa ukatili wa mtu mwovu.

11. Mwovu huwaza moyoni mwake: “Mungu amesahau;ameficha uso wake, haoni kitu!”

12. Inuka, ee Mwenyezi-Mungu, uwaadhibu;usiwasahau wanaodhulumiwa.

13. Ee Mungu, kwa nini mwovu anakudharau,na kusema ati hutamfanya awajibike?

14. Lakini wewe wawaona wenye dhiki na shida;nawe daima uko tayari kuwasaidia.Mnyonge anakutegemea wewe, ee Mungu,wewe umekuwa daima msaada wa yatima.

15. Uzivunje nguvu za mtu mwovu;ukomeshe uovu wake wote, usiwepo tena.

16. Mwenyezi-Mungu ni mfalme milele na milele!Mataifa yasiyomjua yatatoweka nchini mwake.

17. Ee Mwenyezi-Mungu, wapokea dua za mnyonge;wampa moyo na kumtegea sikio.

Kusoma sura kamili Zaburi 10