1. Ee Mwenyezi-Mungu, mbona wasimama mbali?Kwa nini wajificha wakati tumo taabuni?
2. Kwa kiburi waovu wanawatesa maskini;njama zao ziwanase wao wenyewe.
3. Mwovu hujisifia tamaa zake mbaya,mtu wa tamaa hulaani na kumkataa Mwenyezi-Mungu.
4. Katika majivuno yake husema: “Mungu hatagundua.”Mawazo yake yote ni: “Hakuna Mungu.”
5. Njia za mwovu hufanikiwa daima;kwake hukumu zako ziko mbali na mawazo yake,na huwadharau maadui zake wote.