Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 1:1-6 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Heri mtu asiyefuata shauri la waovu,asiyeshiriki njia za wenye dhambi,wala kujumuika na wenye dharau;

2. bali huifurahia sheria ya Mwenyezi-Mungu,na kuitafakari mchana na usiku.

3. Huyo ni kama mti uliopandwa kando ya vijito,unaozaa matunda kwa wakati wake,na majani yake hayanyauki.Kila afanyalo hufanikiwa.

4. Lakini waovu sivyo walivyo;wao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.

5. Kwa hiyo watu waovu wataanguka wakati wa hukumu,wenye dhambi hawatakaa na kusanyiko la waadilifu.

6. Maana Mwenyezi-Mungu huziongoza njia za waadilifu;lakini njia za waovu zitaishia katika maangamizi.

Kusoma sura kamili Zaburi 1