Agano la Kale

Agano Jipya

Yoshua 16:8-10 Biblia Habari Njema (BHN)

8. Kutoka Tapua, mpaka ulikwenda magharibi hadi kijito cha Kana na kuishia bahari ya Mediteranea. Hii ndiyo nchi waliyopewa watu wa kabila la Efraimu kulingana na jamaa zao,

9. pamoja na miji na vijiji ambavyo waliongezewa kutoka kwenye nchi ya kabila la Manase.

10. Waefraimu hawakuwafukuza Wakanaani walioishi Gezeri. Wakanaani hao waliendelea kukaa miongoni mwa watu wa Efraimu mpaka leo, wakiwa watumwa wa kuwafanyia kazi za kulazimishwa.

Kusoma sura kamili Yoshua 16