41. Yoshua aliwashinda watu wote kutoka Kadesh-barnea mpaka Gaza, na kutoka Gosheni mpaka Gibeoni.
42. Aliweza kuitwaa nchi hii yote kwa sababu Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli, aliwapigania Waisraeli.
43. Basi, Yoshua akarudi mpaka kambini huko Gilgali pamoja na Waisraeli wote.