Agano la Kale

Agano Jipya

Yoshua 10:28-30 Biblia Habari Njema (BHN)

28. Siku hiyo Yoshua alipouteka mji wa Makeda, alimuua mfalme wake na wakazi wake wote bila kumbakiza hata mtu mmoja. Alimtendea mfalme wa Makeda kama vile alivyomtendea mfalme wa Yeriko.

29. Kutoka Makeda, Yoshua pamoja na Waisraeli wote walikwenda Libna wakaushambulia.

30. Mwenyezi-Mungu akautia mji huo pamoja na mfalme wao mikononi mwa Waisraeli, wakawaua wakazi wake bila kumbakiza hata mtu mmoja. Walimtendea mfalme wa Libna kama walivyomtendea mfalme wa Yeriko.

Kusoma sura kamili Yoshua 10