Agano la Kale

Agano Jipya

Yona 2:4-10 Biblia Habari Njema (BHN)

4. Nilidhani kwamba nimetengwa nisiwe mbele yako;nisiweze kuliona tena hekalu lako takatifu.

5. Maji yalinizunguka na kunisonga;kilindi kilinifikia kila upande,majani ya baharini yakanifunika kichwa.

6. Niliteremka hadi kwenye misingi ya milima,katika nchi ambayo milango yake imefungwa milele.Lakini wewe, ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu,umenipandisha hai kutoka humo shimoni.

7. Roho yangu ilipoanza kunitoka,nilikukumbuka, ee Mwenyezi-Mungu,sala yangu ikakufikia,katika hekalu lako takatifu.

8. Watu wanaoabudu sanamu za miungu batili,huutupilia mbali uaminifu wao kwako.

9. Lakini mimi, kwa wimbo wa shukrani,nitakutolea sadaka,na kutimiza nadhiri zangu.Mwenyezi-Mungu, ndiye aokoaye.”

10. Basi, Mwenyezi-Mungu akamwamuru yule samaki, naye akamtapika Yona kwenye nchi kavu.

Kusoma sura kamili Yona 2