Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4

Agano la Kale

Agano Jipya

Yona 2 Biblia Habari Njema (BHN)

Sala ya Yona

1. Basi, Yona, akiwa tumboni mwa samaki huyo, akawa akimwomba Mwenyezi-Mungu, Mungu wake,

2. akisema:“Kwa sababu ya taabu yangu,nilikuomba, ee Mwenyezi-Mungu,nawe ukanisikiliza;toka chini kuzimu, nilikulilia,nawe ukasikiliza kilio changu.

3. Ulinitupa katika kilindi, katikati ya bahari,gharika ikanizunguka,mawimbi na gharika vikapita juu yangu.

4. Nilidhani kwamba nimetengwa nisiwe mbele yako;nisiweze kuliona tena hekalu lako takatifu.

5. Maji yalinizunguka na kunisonga;kilindi kilinifikia kila upande,majani ya baharini yakanifunika kichwa.

6. Niliteremka hadi kwenye misingi ya milima,katika nchi ambayo milango yake imefungwa milele.Lakini wewe, ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu,umenipandisha hai kutoka humo shimoni.

7. Roho yangu ilipoanza kunitoka,nilikukumbuka, ee Mwenyezi-Mungu,sala yangu ikakufikia,katika hekalu lako takatifu.

8. Watu wanaoabudu sanamu za miungu batili,huutupilia mbali uaminifu wao kwako.

9. Lakini mimi, kwa wimbo wa shukrani,nitakutolea sadaka,na kutimiza nadhiri zangu.Mwenyezi-Mungu, ndiye aokoaye.”

10. Basi, Mwenyezi-Mungu akamwamuru yule samaki, naye akamtapika Yona kwenye nchi kavu.