1. Basi, Yona, akiwa tumboni mwa samaki huyo, akawa akimwomba Mwenyezi-Mungu, Mungu wake,
2. akisema:“Kwa sababu ya taabu yangu,nilikuomba, ee Mwenyezi-Mungu,nawe ukanisikiliza;toka chini kuzimu, nilikulilia,nawe ukasikiliza kilio changu.
3. Ulinitupa katika kilindi, katikati ya bahari,gharika ikanizunguka,mawimbi na gharika vikapita juu yangu.
4. Nilidhani kwamba nimetengwa nisiwe mbele yako;nisiweze kuliona tena hekalu lako takatifu.
5. Maji yalinizunguka na kunisonga;kilindi kilinifikia kila upande,majani ya baharini yakanifunika kichwa.
6. Niliteremka hadi kwenye misingi ya milima,katika nchi ambayo milango yake imefungwa milele.Lakini wewe, ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu,umenipandisha hai kutoka humo shimoni.
7. Roho yangu ilipoanza kunitoka,nilikukumbuka, ee Mwenyezi-Mungu,sala yangu ikakufikia,katika hekalu lako takatifu.
8. Watu wanaoabudu sanamu za miungu batili,huutupilia mbali uaminifu wao kwako.
9. Lakini mimi, kwa wimbo wa shukrani,nitakutolea sadaka,na kutimiza nadhiri zangu.Mwenyezi-Mungu, ndiye aokoaye.”
10. Basi, Mwenyezi-Mungu akamwamuru yule samaki, naye akamtapika Yona kwenye nchi kavu.