Agano la Kale

Agano Jipya

Yoeli 3:8-13 Biblia Habari Njema (BHN)

8. Watoto wenu wa kiume na wa kike nitawafanya wauzwe kwa watu wa Yuda, nao watawauzia Washeba, watu wa taifa la mbali kabisa. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.

9. “Watangazieni watu wa mataifa jambo hili:Jitayarisheni kwa vita,waiteni mashujaa wenu;askari wote na wakusanyike,waende mbele.

10. Majembe yenu yafueni yawe mapanga,miundu yenu ya kupogolea iwe mikuki.Hata aliye dhaifu na aseme:‘Mimi pia ni shujaa’.

11. Njoni haraka, enyi mataifa yote jirani,kusanyikeni huko bondeni.”Ee Mwenyezi-Mungu!Teremsha askari wako dhidi yao!

12. “Haya mataifa na yajiweke tayari;yaje kwenye bonde liitwalo:‘Mwenyezi-Mungu Ahukumu’.Huko, mimi Mwenyezi-Mungu,nitaketi kuyahukumu mataifa yote ya jirani.

13. Haya! Chukueni mundu wa kuvuna,kwani sasa ni wakati wa mavuno.Ingieni! Wapondeni kama zabibuambazo zimejaza shinikizo.Uovu wao umepita kiasikama mapipa yanayofurika.”

Kusoma sura kamili Yoeli 3