Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3

Agano la Kale

Agano Jipya

Yoeli 3 Biblia Habari Njema (BHN)

Mungu atayahukumu mataifa

1. “Wakati huo na siku hizonitakapoirekebisha hali ya Yuda na Yerusalemu,

2. nitayakusanya mataifa yote,niyapeleke katika bonde liitwalo,‘Mwenyezi-Mungu Ahukumu.Huko nitayahukumu mataifa hayo,kwa mambo yaliyowatendea watu wangu Israeli,hao walio mali yangu mimi mwenyewe.Maana waliwatawanya miongoni mwa mataifa,waligawa nchi yangu

3. na kugawana watu wangu kwa kura.Waliwauza wavulana ili kulipia malaya,na wasichana ili kulipia divai.

4. “Mnataka kunifanya nini enyi Tiro na Sidoni na maeneo yote ya Filistia? Je, mna kisasi nami mnachotaka kulipiza? Kama mnalipiza kisasi, mimi nitawalipizeni mara moja!

5. Mmechukua fedha na dhahabu yangu, na kuvibeba vitu vyangu vya thamani hadi kwenye mahekalu yenu.

6. Mmewapeleka watu wa Yuda na Yerusalemu mbali na nchi yao, mkawauza kwa Wagiriki.

7. Sasa, nitawarudisha watu wangu kutoka huko mlikowauza. Nitawalipizeni kisasi kwa yote mliyowatendea.

8. Watoto wenu wa kiume na wa kike nitawafanya wauzwe kwa watu wa Yuda, nao watawauzia Washeba, watu wa taifa la mbali kabisa. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.

9. “Watangazieni watu wa mataifa jambo hili:Jitayarisheni kwa vita,waiteni mashujaa wenu;askari wote na wakusanyike,waende mbele.

10. Majembe yenu yafueni yawe mapanga,miundu yenu ya kupogolea iwe mikuki.Hata aliye dhaifu na aseme:‘Mimi pia ni shujaa’.

11. Njoni haraka, enyi mataifa yote jirani,kusanyikeni huko bondeni.”Ee Mwenyezi-Mungu!Teremsha askari wako dhidi yao!

12. “Haya mataifa na yajiweke tayari;yaje kwenye bonde liitwalo:‘Mwenyezi-Mungu Ahukumu’.Huko, mimi Mwenyezi-Mungu,nitaketi kuyahukumu mataifa yote ya jirani.

13. Haya! Chukueni mundu wa kuvuna,kwani sasa ni wakati wa mavuno.Ingieni! Wapondeni kama zabibuambazo zimejaza shinikizo.Uovu wao umepita kiasikama mapipa yanayofurika.”

14. Wanafika makundi kwa makundikwenye bonde la Hukumu,maana siku ya Mwenyezi-Mungu imekaribia.

15. Jua na mwezi vinatiwa giza,na nyota zimeacha kuangaza.

Mungu atawabariki watu wake

16. Mwenyezi-Mungu ananguruma huko Siyoni;sauti yake inavuma kutoka Yerusalemu;mbingu na dunia vinatetemeka.Lakini Mwenyezi-Mungu ni kimbilio la watu wake,ni ngome ya usalama kwa Waisraeli.

17. “Hapo, ewe Israeli,utajua kwamba mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wako,nakaa Siyoni, mlima wangu mtakatifu,Yerusalemu utakuwa mji mtakatifu;na wageni hawatapita tena humo.

18. “Wakati huo, milima itatiririka divai mpya,na vilima vitatiririka maziwa.Vijito vyote vya Yuda vitajaa maji;chemchemi itatokea nyumbani mwa Mwenyezi-Mungu,na kulinywesha bonde la Shitimu.

19. “Misri itakuwa mahame,Edomu itakuwa jangwa tupu,kwa sababu waliwashambulia watu wa Yudawakawaua watu wasio na hatia.

20. Bali Yuda itakaliwa milele,na Yerusalemu kizazi hata kizazi.

21. Nitawaadhibu waliomwaga damu ya watu wa Yudawala sitawaachia wenye hatia.Mimi, Mwenyezi-Mungu nakaa Siyoni.”