Agano la Kale

Agano Jipya

Yoeli 3:11-21 Biblia Habari Njema (BHN)

11. Njoni haraka, enyi mataifa yote jirani,kusanyikeni huko bondeni.”Ee Mwenyezi-Mungu!Teremsha askari wako dhidi yao!

12. “Haya mataifa na yajiweke tayari;yaje kwenye bonde liitwalo:‘Mwenyezi-Mungu Ahukumu’.Huko, mimi Mwenyezi-Mungu,nitaketi kuyahukumu mataifa yote ya jirani.

13. Haya! Chukueni mundu wa kuvuna,kwani sasa ni wakati wa mavuno.Ingieni! Wapondeni kama zabibuambazo zimejaza shinikizo.Uovu wao umepita kiasikama mapipa yanayofurika.”

14. Wanafika makundi kwa makundikwenye bonde la Hukumu,maana siku ya Mwenyezi-Mungu imekaribia.

15. Jua na mwezi vinatiwa giza,na nyota zimeacha kuangaza.

16. Mwenyezi-Mungu ananguruma huko Siyoni;sauti yake inavuma kutoka Yerusalemu;mbingu na dunia vinatetemeka.Lakini Mwenyezi-Mungu ni kimbilio la watu wake,ni ngome ya usalama kwa Waisraeli.

17. “Hapo, ewe Israeli,utajua kwamba mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wako,nakaa Siyoni, mlima wangu mtakatifu,Yerusalemu utakuwa mji mtakatifu;na wageni hawatapita tena humo.

18. “Wakati huo, milima itatiririka divai mpya,na vilima vitatiririka maziwa.Vijito vyote vya Yuda vitajaa maji;chemchemi itatokea nyumbani mwa Mwenyezi-Mungu,na kulinywesha bonde la Shitimu.

19. “Misri itakuwa mahame,Edomu itakuwa jangwa tupu,kwa sababu waliwashambulia watu wa Yudawakawaua watu wasio na hatia.

20. Bali Yuda itakaliwa milele,na Yerusalemu kizazi hata kizazi.

21. Nitawaadhibu waliomwaga damu ya watu wa Yudawala sitawaachia wenye hatia.Mimi, Mwenyezi-Mungu nakaa Siyoni.”

Kusoma sura kamili Yoeli 3