Agano la Kale

Agano Jipya

Yoeli 2:3-15 Biblia Habari Njema (BHN)

3. Kama vile moto uteketezavyojeshi hilo laharibu kila kitu mbele yakena kuacha nyuma kila kitu kinateketezwa;kabla hawajapita, nchi ni kama bustani ya Edeni,lakini wakisha pita, ni jangwa tupu.Hakuna kiwezacho kuwaepa!

4. Wanaonekana kama farasi,wanashambulia kama farasi wa vita,

5. Wanaporukaruka kwenye vilele vya milima,wanarindima kama magari ya farasi,wanavuma kama mabua makavu motoni.Wamejipanga kama jeshi kubwatayari kabisa kufanya vita.

6. Wakaribiapo, watu hujaa hofu,nyuso zao zinawaiva.

7. Wanashambulia kama mashujaa wa vita;kuta wanazipanda kama wanajeshi.Wote wanakwenda mbele moja kwa moja,bila hata mmoja wao kubadilisha njia.

8. Hakuna amsukumaye mwenziwe;kila mmoja anafuata mkondo wake.Wanapita kati ya vizuizi vya silaha,wala hakuna kiwezacho kuwazuia.

9. Wanauvamia mji,wanapiga mbio ukutani;wanaziparamia nyumba na kuingia,wanapenya madirishani kama wezi.

10. Nchi inatetemeka mbele yao,mbingu zinatikisika.Jua na mwezi vyatiwa giza,nazo nyota zinaacha kuangaza.

11. Mwenyezi-Mungu anaamuru jeshi lake kwa sauti;askari wake ni wengi mno,wanaomtii hawahesabiki.2Siku ya Mwenyezi-Mungu kweli ni kuu na ya kutisha sana!Nani atakayeweza kuistahimili?

12. “Lakini hata sasa,”nasema mimi Mwenyezi-Mungu,“Nirudieni kwa moyo wote,kwa kufunga, kulia na kuomboleza.

13. Msirarue mavazi yenu kuonesha huzunibali nirudieni kwa moyo wa toba.”Mrudieni Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu;yeye amejaa neema na huruma;hakasiriki upesi, ni mwingi wa fadhili;daima yu tayari kuacha kuadhibu.

14. Huenda Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu, atabadili niana kuwapeni baraka ya mazao,mkamtolea sadaka za nafaka na kinywaji.

15. Pigeni tarumbeta huko Siyoni!Toeni amri watu wafunge;itisheni mkutano wa kidini.

Kusoma sura kamili Yoeli 2