Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3

Agano la Kale

Agano Jipya

Yoeli 2 Biblia Habari Njema (BHN)

Nzige: Onyo juu ya siku ya Mwenyezi-Mungu

1. Pigeni tarumbeta huko Siyoni;pigeni baragumu juu ya mlima mtakatifu!Tetemekeni enyi wakazi wa Yuda,maana siku ya Mwenyezi-Mungu inakuja,naam, siku hiyo iko karibu!

2. Hiyo ni siku ya giza na huzuni;siku ya mawingu na giza nene.Jeshi kubwa la nzige linakaribiakama giza linalotanda milimani.Namna hiyo haijapata kuweko kamwewala haitaonekana tenakatika vizazi vyote vijavyo.

3. Kama vile moto uteketezavyojeshi hilo laharibu kila kitu mbele yakena kuacha nyuma kila kitu kinateketezwa;kabla hawajapita, nchi ni kama bustani ya Edeni,lakini wakisha pita, ni jangwa tupu.Hakuna kiwezacho kuwaepa!

4. Wanaonekana kama farasi,wanashambulia kama farasi wa vita,

5. Wanaporukaruka kwenye vilele vya milima,wanarindima kama magari ya farasi,wanavuma kama mabua makavu motoni.Wamejipanga kama jeshi kubwatayari kabisa kufanya vita.

6. Wakaribiapo, watu hujaa hofu,nyuso zao zinawaiva.

7. Wanashambulia kama mashujaa wa vita;kuta wanazipanda kama wanajeshi.Wote wanakwenda mbele moja kwa moja,bila hata mmoja wao kubadilisha njia.

8. Hakuna amsukumaye mwenziwe;kila mmoja anafuata mkondo wake.Wanapita kati ya vizuizi vya silaha,wala hakuna kiwezacho kuwazuia.

9. Wanauvamia mji,wanapiga mbio ukutani;wanaziparamia nyumba na kuingia,wanapenya madirishani kama wezi.

10. Nchi inatetemeka mbele yao,mbingu zinatikisika.Jua na mwezi vyatiwa giza,nazo nyota zinaacha kuangaza.

11. Mwenyezi-Mungu anaamuru jeshi lake kwa sauti;askari wake ni wengi mno,wanaomtii hawahesabiki.2Siku ya Mwenyezi-Mungu kweli ni kuu na ya kutisha sana!Nani atakayeweza kuistahimili?

Wito wa toba

12. “Lakini hata sasa,”nasema mimi Mwenyezi-Mungu,“Nirudieni kwa moyo wote,kwa kufunga, kulia na kuomboleza.

13. Msirarue mavazi yenu kuonesha huzunibali nirudieni kwa moyo wa toba.”Mrudieni Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu;yeye amejaa neema na huruma;hakasiriki upesi, ni mwingi wa fadhili;daima yu tayari kuacha kuadhibu.

14. Huenda Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu, atabadili niana kuwapeni baraka ya mazao,mkamtolea sadaka za nafaka na kinywaji.

15. Pigeni tarumbeta huko Siyoni!Toeni amri watu wafunge;itisheni mkutano wa kidini.

16. Wakusanyeni watu wote,wawekeni watu wakfu.Waleteni wazee,wakusanyeni watoto,hata watoto wanyonyao.Bwana arusi na bibi arusina watoke vyumbani mwao.

17. Kati ya madhabahu na lango la hekalu,makuhani, wahudumu wa Mwenyezi-Mungu,walie na kuomba wakisema:“Wahurumie watu wako, ee Mwenyezi-Mungu.Usiyaache mataifa mengine yatudharauna kutudhihaki yakisema,‘Yuko wapi basi Mungu wao?’”

Mungu ataifanikisha nchi

18. Ndipo Mwenyezi-Mungu akaipenda nchi yakeakawahurumia watu wake.

19. Alisikiliza, akajibu sala zao; akasema,“Sasa nitawapeni tena nafaka,sitawafanya mdharauliwe tena na mataifa.

20. Nitawaondoa hao adui watokao kaskazini,nitawafukuza mpaka jangwani;askari wa mbele nitawatupa katika Bahari ya Chumvina wale wa nyuma katika Bahari ya Mediteranea.Watatoa uvundo na harufu mbaya,hao ambao wamefanya maovu makubwa.

21. “Usiogope, ewe nchi,bali furahi na kushangilia,maana Mwenyezi-Mungu ametenda makuu.

22. Msiogope, enyi wanyama.malisho ya nyikani yamekuwa mazuri,miti inazaa matunda yake,mizabibu na mitini zinazaa kwa wingi.

23. “Furahini, enyi watu wa Siyoni,shangilieni kwa sababu ya Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu,maana amewapeni mvua za masika,amewapeni mvua ya kutosha:Mvua za masika na mvua za vuli kama hapo awali.

24. Mahali pa kupuria patajaa nafaka,mashinikizo yatafurika divai na mafuta.

25. Nitawarudishia miaka ile iliyoliwa na nzige,kila kitu kilicholiwa na tunutu, parare na matumatu,hilo jeshi kubwa nililowaletea!

26. Mtapata chakula kingi na kutosheka;mtalisifu jina la Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu,aliyewatendea mambo ya ajabu.Watu wangu, kamwe hawatadharauliwa tena.

27. Mtatambua kwamba mimi nimo miongoni mwenu,enyi Waisraeli;kwamba mimi Mwenyezi-Mungu,ndimi Mungu wenu wala hakuna mwingine.Watu wangu, kamwe hawatadharauliwa tena.

Siku ya Mwenyezi-Mungu

28. “Kisha hapo baadayenitaimimina roho yangu juu ya binadamu wote.Watoto wenu wa kike na wa kiume watatabiri,wazee wenu wataota ndoto,na vijana wenu wataona maono.

29. Hata juu ya watumishi wa kiume na wa kike,nitaimimina roho yangu wakati huo.

30. “Nitatoa ishara mbinguni na duniani;kutakuwa na damu, moto na minara ya moshi.

31. Jua litatiwa giza,na mwezi utakuwa mwekundu kama damu,kabla ya kufika siku ya Mwenyezi-Mungu,siku iliyo kuu na ya kutisha.

32. Hapo watu wote watakaoomba kwa jina la Mwenyezi-Mungu wataokolewa.Maana katika mlima Siyoni na Yerusalemu,watakuwako watu watakaosalimika,kama nilivyosema mimi Mwenyezi-Mungu.