Agano la Kale

Agano Jipya

Yoeli 2:21-25 Biblia Habari Njema (BHN)

21. “Usiogope, ewe nchi,bali furahi na kushangilia,maana Mwenyezi-Mungu ametenda makuu.

22. Msiogope, enyi wanyama.malisho ya nyikani yamekuwa mazuri,miti inazaa matunda yake,mizabibu na mitini zinazaa kwa wingi.

23. “Furahini, enyi watu wa Siyoni,shangilieni kwa sababu ya Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu,maana amewapeni mvua za masika,amewapeni mvua ya kutosha:Mvua za masika na mvua za vuli kama hapo awali.

24. Mahali pa kupuria patajaa nafaka,mashinikizo yatafurika divai na mafuta.

25. Nitawarudishia miaka ile iliyoliwa na nzige,kila kitu kilicholiwa na tunutu, parare na matumatu,hilo jeshi kubwa nililowaletea!

Kusoma sura kamili Yoeli 2