1. Pigeni tarumbeta huko Siyoni;pigeni baragumu juu ya mlima mtakatifu!Tetemekeni enyi wakazi wa Yuda,maana siku ya Mwenyezi-Mungu inakuja,naam, siku hiyo iko karibu!
2. Hiyo ni siku ya giza na huzuni;siku ya mawingu na giza nene.Jeshi kubwa la nzige linakaribiakama giza linalotanda milimani.Namna hiyo haijapata kuweko kamwewala haitaonekana tenakatika vizazi vyote vijavyo.
3. Kama vile moto uteketezavyojeshi hilo laharibu kila kitu mbele yakena kuacha nyuma kila kitu kinateketezwa;kabla hawajapita, nchi ni kama bustani ya Edeni,lakini wakisha pita, ni jangwa tupu.Hakuna kiwezacho kuwaepa!