Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 38:8-25 Biblia Habari Njema (BHN)

8. Ni nani aliyeyafunga mafuriko ya bahariwakati yalipozuka na kuvuma kutoka vilindini?

9. Mimi ndiye niliyeifunika bahari kwa mawinguna kuiviringishia giza nene.

10. Niliiwekea bahari mipaka,nikaizuia kwa makomeo na milango,

11. nikaiambia: ‘Mwisho wako ni hapa, si zaidi!Mawimbi yako ya nguvu yatakomea hapa!’

12. “Yobu, tangu uzaliwe umewahi kuamuru kupambazuke?na kulifanya pambazuko lijue mahali pake,

13. ili lipate kuikamata dunia kwa pembe zakena kuwatimulia mbali waovu waliomo?

14. Dunia hugeuka na kupata rangi kama vazi;kama udongo wa mfinyanzi unavyogeuzwa na mhuri.

15. Lakini waovu watanyimwa mwanga wao,mkono wanaonyosha kupiga watu utavunjwa.

16. “Je, umepata kufika kwenye chemchemi za bahari?au kutembea juu ya sakafu ya kilindi cha bahari?

17. Je, umewahi kuoneshwa malango ya kifo,au kuyaona malango ya makazi ya giza nene?

18. Je, wajua ukubwa wa dunia?Niambie kama unajua haya yote.

19. “Je, makao ya mwanga yako wapi?Nyumbani kwa giza ni wapi,

20. ili upate kulipeleka kwenye makao yake,na kuifahamu njia ya kwenda huko kwake.

21. Wewe unapaswa kujua,wewe ambaye umekwisha ishi miaka mingi!

22. “Je, umewahi kuingia katika bohari za theluji,au kuona bohari za mvua ya mawe

23. ambavyo nimevihifadhi kwa ajili ya wakati wa fujo,kwa ajili ya siku ya mapigano na vita?

24. Ipi njia ya kwenda mahali mwanga unapogawanywa,au huko kunakotoka upepo wa mashariki ukasambazwa duniani?

25. “Nani aliyechora angani njia kwa ajili ya mvua?Nani aliyeionesha radi njia yake mawinguni,

Kusoma sura kamili Yobu 38