Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 38:33-39 Biblia Habari Njema (BHN)

33. Je, wazijua kanuni zinazotawala mbingu;Je, waweza kuzipangia taratibu zao duniani?

34. “Je, waweza kupaza sauti na kuyaamuru mawinguyakufunike kwa mtiririko wa mvua?

35. Je, wewe ukiamuru umeme umulike,utakujia na kusema: ‘Nipo hapa?’

36. Ni nani aliyemjulisha kwarara kujaa kwa mto Niliau aliyemwambia jogoo kwamba mvua inakuja?

37. Nani mwenye akili ya kuweza kuhesabu mawingu,au kuinamisha viriba vya maji huko mbinguni?

38. ili vumbi duniani igandamanena udongo ushikamane na kuwa matope?

39. “Je, waweza kumwindia simba mawindo yakeau kuishibisha hamu ya wana simba;

Kusoma sura kamili Yobu 38