Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 38:30-41 Biblia Habari Njema (BHN)

30. Maji hugeuka kuwa magumu kama jiwe,na uso wa bahari ukaganda.

31. “Angalia makundi ya nyota:Je, unaweza kuifunga minyororo Kilimia,au kuvilegeza vifungo vya Orioni?

32. Je, waweza kuziongoza nyota katika majira yake,au kumwongoza Dubu pamoja na watoto wake?

33. Je, wazijua kanuni zinazotawala mbingu;Je, waweza kuzipangia taratibu zao duniani?

34. “Je, waweza kupaza sauti na kuyaamuru mawinguyakufunike kwa mtiririko wa mvua?

35. Je, wewe ukiamuru umeme umulike,utakujia na kusema: ‘Nipo hapa?’

36. Ni nani aliyemjulisha kwarara kujaa kwa mto Niliau aliyemwambia jogoo kwamba mvua inakuja?

37. Nani mwenye akili ya kuweza kuhesabu mawingu,au kuinamisha viriba vya maji huko mbinguni?

38. ili vumbi duniani igandamanena udongo ushikamane na kuwa matope?

39. “Je, waweza kumwindia simba mawindo yakeau kuishibisha hamu ya wana simba;

40. wanapojificha mapangoni mwao,au kulala mafichoni wakiotea?

41. Ni nani awapaye kunguru chakula chao,makinda yao yanaponililia mimi Mungu,na kurukaruka huku na huko kwa njaa?

Kusoma sura kamili Yobu 38