29. Je, barafu ilitoka tumboni kwa nani?Nani aliyeizaa theluji?
30. Maji hugeuka kuwa magumu kama jiwe,na uso wa bahari ukaganda.
31. “Angalia makundi ya nyota:Je, unaweza kuifunga minyororo Kilimia,au kuvilegeza vifungo vya Orioni?
32. Je, waweza kuziongoza nyota katika majira yake,au kumwongoza Dubu pamoja na watoto wake?
33. Je, wazijua kanuni zinazotawala mbingu;Je, waweza kuzipangia taratibu zao duniani?
34. “Je, waweza kupaza sauti na kuyaamuru mawinguyakufunike kwa mtiririko wa mvua?
35. Je, wewe ukiamuru umeme umulike,utakujia na kusema: ‘Nipo hapa?’
36. Ni nani aliyemjulisha kwarara kujaa kwa mto Niliau aliyemwambia jogoo kwamba mvua inakuja?
37. Nani mwenye akili ya kuweza kuhesabu mawingu,au kuinamisha viriba vya maji huko mbinguni?