Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 38:24-35 Biblia Habari Njema (BHN)

24. Ipi njia ya kwenda mahali mwanga unapogawanywa,au huko kunakotoka upepo wa mashariki ukasambazwa duniani?

25. “Nani aliyechora angani njia kwa ajili ya mvua?Nani aliyeionesha radi njia yake mawinguni,

26. ikasababisha mvua kunyesha nchini kusikoishi mtuna jangwani ambako hakuna mtu,

27. ili kuiburudisha nchi kavu na kamena kuifanya iote nyasi?

28. “Je, mvua ina baba?Au nani ameyazaa matone ya umande?

29. Je, barafu ilitoka tumboni kwa nani?Nani aliyeizaa theluji?

30. Maji hugeuka kuwa magumu kama jiwe,na uso wa bahari ukaganda.

31. “Angalia makundi ya nyota:Je, unaweza kuifunga minyororo Kilimia,au kuvilegeza vifungo vya Orioni?

32. Je, waweza kuziongoza nyota katika majira yake,au kumwongoza Dubu pamoja na watoto wake?

33. Je, wazijua kanuni zinazotawala mbingu;Je, waweza kuzipangia taratibu zao duniani?

34. “Je, waweza kupaza sauti na kuyaamuru mawinguyakufunike kwa mtiririko wa mvua?

35. Je, wewe ukiamuru umeme umulike,utakujia na kusema: ‘Nipo hapa?’

Kusoma sura kamili Yobu 38