Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 38:21-27 Biblia Habari Njema (BHN)

21. Wewe unapaswa kujua,wewe ambaye umekwisha ishi miaka mingi!

22. “Je, umewahi kuingia katika bohari za theluji,au kuona bohari za mvua ya mawe

23. ambavyo nimevihifadhi kwa ajili ya wakati wa fujo,kwa ajili ya siku ya mapigano na vita?

24. Ipi njia ya kwenda mahali mwanga unapogawanywa,au huko kunakotoka upepo wa mashariki ukasambazwa duniani?

25. “Nani aliyechora angani njia kwa ajili ya mvua?Nani aliyeionesha radi njia yake mawinguni,

26. ikasababisha mvua kunyesha nchini kusikoishi mtuna jangwani ambako hakuna mtu,

27. ili kuiburudisha nchi kavu na kamena kuifanya iote nyasi?

Kusoma sura kamili Yobu 38