Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 31:5-11 Biblia Habari Njema (BHN)

5. “Kama nimeishi kwa kufuata uongo,kama nimekuwa mbioni kudanganya watu,

6. Mungu na anipime katika mizani ya haki,naye ataona kwamba sina hatia.

7. Kama hatua zangu zimepotoka,moyo wangu ukafuata tamaa za macho yangu;kama mikono yangu imechafuliwa na dhambi,

8. jasho langu na liliwe na mtu mwingine,mazao yangu shambani na yangolewe.

9. “Kama moyo wangu umevutwa kwa mke wa mtu,kama nimenyemelea mlangoni kwa jirani yangu,

10. basi, mke wangu na ampikie mume mwingine,na wanaume wengine wamtumie.

11. Jambo hilo ni kosa kuu la jinai,uovu ambao hakimu lazima atoe adhabu.

Kusoma sura kamili Yobu 31