Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 31:31-35 Biblia Habari Njema (BHN)

31. Watumishi wangu wote wanasema wazikila mgeni amekaribishwa nyumbani mwangu.

32. Msafiri hakulala nje ya nyumba yangu,nilimfungulia mlango mpita njia.

33. Je nimeficha makosa yangu kama wengine?Je nimekataa kukiri dhambi zangu?

34. Sijaogopa kusimama mbele ya umati wa watu,wala kukaa kimya au kujifungia ndani,eti kwa kuogopa kutishwa na dharau zao.

35. Laiti angekuwapo mtu wa kunisikiliza!Naweza kutia sahihi yangu katika kila nilichosema.Namwambia Mungu Mwenye Nguvu anijibu!Laiti mashtaka wanayonitolea maadui zangu yangeandikwa!

Kusoma sura kamili Yobu 31