Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 31:26-35 Biblia Habari Njema (BHN)

26. Kama nimeliangalia jua likiangaza,na mwezi ukipita katika uzuri wake,

27. na moyo wangu ukashawishika kuviabudu,nami nikaibusu mikono yangu kwa heshima yake,

28. huo pia ungekuwa uovu wa kuadhibiwa na mahakimumaana ningekuwa mwongo mbele ya Mungu aliye juu.

29. “Je, nimefurahia kuangamia kwa adui yangu,au kufurahi alipopatwa na maafa?

30. La! Sikuruhusu kinywa changu kumtakia mabaya,kwa kumlaani ili afe.

31. Watumishi wangu wote wanasema wazikila mgeni amekaribishwa nyumbani mwangu.

32. Msafiri hakulala nje ya nyumba yangu,nilimfungulia mlango mpita njia.

33. Je nimeficha makosa yangu kama wengine?Je nimekataa kukiri dhambi zangu?

34. Sijaogopa kusimama mbele ya umati wa watu,wala kukaa kimya au kujifungia ndani,eti kwa kuogopa kutishwa na dharau zao.

35. Laiti angekuwapo mtu wa kunisikiliza!Naweza kutia sahihi yangu katika kila nilichosema.Namwambia Mungu Mwenye Nguvu anijibu!Laiti mashtaka wanayonitolea maadui zangu yangeandikwa!

Kusoma sura kamili Yobu 31