Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 31:24-30 Biblia Habari Njema (BHN)

24. “Je, tumaini langu nimeliweka katika dhahabu,au, nimeiambia dhahabu safi, ‘Wewe ni usalama wangu?’

25. Je, nimepata kufurahia wingi wa utajiri wanguau kujivunia mapato ya mikono yangu?

26. Kama nimeliangalia jua likiangaza,na mwezi ukipita katika uzuri wake,

27. na moyo wangu ukashawishika kuviabudu,nami nikaibusu mikono yangu kwa heshima yake,

28. huo pia ungekuwa uovu wa kuadhibiwa na mahakimumaana ningekuwa mwongo mbele ya Mungu aliye juu.

29. “Je, nimefurahia kuangamia kwa adui yangu,au kufurahi alipopatwa na maafa?

30. La! Sikuruhusu kinywa changu kumtakia mabaya,kwa kumlaani ili afe.

Kusoma sura kamili Yobu 31