Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 3:17-26 Biblia Habari Njema (BHN)

17. Huko kwa wafu waovu hawamsumbui mtu,huko wachovu hupumzika.

18. Huko wafungwa hustarehe pamoja,hawaisikii kamwe sauti ya mnyapara.

19. Wakubwa na wadogo wako huko,nao watumwa wamepata uhuru mbali na bwana zao.

20. Ya nini kumjalia nuru yule aliye taabuni;na uhai yule aliye na huzuni moyoni?

21. Mtu atamaniye kifo lakini hafi;hutafuta kifo kuliko hazina iliyofichika.

22. Mtu kama huyo atashangilia mno na kufurahi,atafurahi atakapokufa na kuzikwa!

23. Ya nini kumjalia uhai mtu ambaye njia zake zimefungwa,mtu ambaye Mungu amemwekea kizuizi?

24. Kwa maana kusononeka ndio mkate wangu,kupiga kite kwangu kunatiririka mithili ya maji.

25. Kile ninachokiogopa kimenipata,ninachokihofia ndicho kilichonikumba.

26. Sina amani wala utulivu;sipumziki, taabu imenijia.”

Kusoma sura kamili Yobu 3