7. Kwa nini basi waovu wanaishi bado?Mbona nguvu zao zaongezeka hata uzeeni?
8. Huwaona watoto wao wakifanikiwa;na wazawa wao wakipata nguvu.
9. Kwao kila kitu ni salama bila hofu;wala kiboko cha Mungu hakiwafikii.
10. Naam, ng'ombe wao wote huongezeka,huzaa bila matatizo yoyote.
11. Watoto wao wachanga huwatembeza kama kundi;na watoto wao hucheza ngoma;
12. hucheza muziki wa ngoma na vinubi,na kufurahia sauti ya filimbi.
13. Huishi maisha ya fanakakisha hushuka kwa amani kuzimu.
14. Humwambia Mungu, ‘Usitusumbue!Hatutaki kujua matakwa yako.