Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 21:7-14 Biblia Habari Njema (BHN)

7. Kwa nini basi waovu wanaishi bado?Mbona nguvu zao zaongezeka hata uzeeni?

8. Huwaona watoto wao wakifanikiwa;na wazawa wao wakipata nguvu.

9. Kwao kila kitu ni salama bila hofu;wala kiboko cha Mungu hakiwafikii.

10. Naam, ng'ombe wao wote huongezeka,huzaa bila matatizo yoyote.

11. Watoto wao wachanga huwatembeza kama kundi;na watoto wao hucheza ngoma;

12. hucheza muziki wa ngoma na vinubi,na kufurahia sauti ya filimbi.

13. Huishi maisha ya fanakakisha hushuka kwa amani kuzimu.

14. Humwambia Mungu, ‘Usitusumbue!Hatutaki kujua matakwa yako.

Kusoma sura kamili Yobu 21