Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 21:3-16 Biblia Habari Njema (BHN)

3. Nivumilieni, nami nitasema,na nikisha sema endeleeni kunidhihaki.

4. Je, mimi namlalamikia binadamu?Ya nini basi, nikose uvumilivu?

5. Niangalieni, nanyi mshangae,fumbeni mdomo kwa mkono.

6. Nikifikiri yaliyonipata nafadhaikanafa ganzi mwilini kwa hofu.

7. Kwa nini basi waovu wanaishi bado?Mbona nguvu zao zaongezeka hata uzeeni?

8. Huwaona watoto wao wakifanikiwa;na wazawa wao wakipata nguvu.

9. Kwao kila kitu ni salama bila hofu;wala kiboko cha Mungu hakiwafikii.

10. Naam, ng'ombe wao wote huongezeka,huzaa bila matatizo yoyote.

11. Watoto wao wachanga huwatembeza kama kundi;na watoto wao hucheza ngoma;

12. hucheza muziki wa ngoma na vinubi,na kufurahia sauti ya filimbi.

13. Huishi maisha ya fanakakisha hushuka kwa amani kuzimu.

14. Humwambia Mungu, ‘Usitusumbue!Hatutaki kujua matakwa yako.

15. Mungu Mwenye Nguvu ni nini hata tumtumikie?Tunapata faida gani tukimwomba dua?’

16. Kufanikiwa kwao si kuko mikononi mwao,wakiwa wamemweka Mungu mbali na mipango yao?

Kusoma sura kamili Yobu 21