Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 21:19-28 Biblia Habari Njema (BHN)

19. “Nyinyi mwasema, ‘Mungu amewawekea watoto waoadhabu ya watu hao waovu.’Kwa nini hawalipizi wao wenyewe, wapate kutambua!

20. Waone wao wenyewe wakiangamia;waone wenyewe ghadhabu ya Mungu mwenye nguvu.

21. Maana wakifa watajali nini juu ya wazawa wao,wakati siku zao zitakapokuwa zimefika mwisho?

22. Je, binadamu aweza kumfunza Mungu maarifa,Mungu ambaye huwahukumu wakazi wa mbinguni?

23. “Mtu hufa katika kilele cha ufanisi wake,akiwa katika raha mustarehe na salama;

24. amejaa mafuta tele mwilini,na mifupa yake ikiwa bado na nguvu.

25. Mwingine hufa na huzuni kubwa moyoni,akiwa hajawahi kuonja lolote jema.

26. Hata hivyo, wote hufa na kuzikwa,wote hufunikwa na mabuu.

27. “Sikilizeni! Mimi nayajua mawazo yenu yote,na mipango yenu ya kunidharau.

28. Eti mwauliza, ‘Iko wapi nyumba ya mkuu?Iko wapi nyumba alimoishi mwovu?’

Kusoma sura kamili Yobu 21