Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 21:1-9 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Kisha Yobu akajibu:

2. “Sikilizeni kwa makini maneno yangu;na hiyo iwe ndiyo faraja yenu.

3. Nivumilieni, nami nitasema,na nikisha sema endeleeni kunidhihaki.

4. Je, mimi namlalamikia binadamu?Ya nini basi, nikose uvumilivu?

5. Niangalieni, nanyi mshangae,fumbeni mdomo kwa mkono.

6. Nikifikiri yaliyonipata nafadhaikanafa ganzi mwilini kwa hofu.

7. Kwa nini basi waovu wanaishi bado?Mbona nguvu zao zaongezeka hata uzeeni?

8. Huwaona watoto wao wakifanikiwa;na wazawa wao wakipata nguvu.

9. Kwao kila kitu ni salama bila hofu;wala kiboko cha Mungu hakiwafikii.

Kusoma sura kamili Yobu 21