18. Huwavua wafalme vilemba vyao;na kuwafunga viunoni kamba za wafungwa;
19. Huwaacha makuhani waende uchi;na kuwaangusha wenye nguvu.
20. Huwanyanganya washauri kipawa chao cha kuongea,huwapokonya wazee hekima yao.
21. Huwamwagia wakuu aibu,huwaondolea wenye uwezo nguvu zao.
22. Huvifunua vilindi vya giza,na kuleta mwangani yaliyokuwa gizani.