Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 12:13-18 Biblia Habari Njema (BHN)

13. Lakini hekima na uwezo ni vyake Mungu,yeye ana maarifa na ujuzi.

14. Akibomoa, hakuna awezaye kujenga upya;akimfunga mtu, hakuna awezaye kumfungua.

15. Akizuia mvua, twapata ukame;akiifungulia, nchi hupata mafuriko.

16. Yeye ana nguvu na hekima;wanaodanganywa na wanaodanganya ni wake.

17. Huwaacha washauri waende zao uchi,huwafanya waamuzi kuwa wapumbavu.

18. Huwavua wafalme vilemba vyao;na kuwafunga viunoni kamba za wafungwa;

Kusoma sura kamili Yobu 12