Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 11:2-7 Biblia Habari Njema (BHN)

2. “Je, wingi huu wa maneno uachwe tu bila kujibiwa?Je, mtu wa maneno mengi aonesha kuwa hana hatia?

3. Je, kuropoka kwako kutanyamazisha watu?Na kama ukidhihaki, je, hamna atakayekuaibisha?

4. Wewe wadai: ‘Ninachosema ni kweli,naam, sina lawama mbele ya Mungu.’

5. Laiti Mungu angefungua kinywa chakeakatoa sauti yake kukujibu!

6. Angekueleza siri za hekima,maana yeye ni mwingi wa maarifa.Jua kwamba Mungu hakuhesabu makosa yako yote.

7. “Je, unaweza kugundua siri zake Munguna kujua ukomo wake yeye Mungu mwenye nguvu?

Kusoma sura kamili Yobu 11