1. Kisha Sofari, Mnaamathi, akamjibu Yobu:
2. “Je, wingi huu wa maneno uachwe tu bila kujibiwa?Je, mtu wa maneno mengi aonesha kuwa hana hatia?
3. Je, kuropoka kwako kutanyamazisha watu?Na kama ukidhihaki, je, hamna atakayekuaibisha?
4. Wewe wadai: ‘Ninachosema ni kweli,naam, sina lawama mbele ya Mungu.’
5. Laiti Mungu angefungua kinywa chakeakatoa sauti yake kukujibu!
6. Angekueleza siri za hekima,maana yeye ni mwingi wa maarifa.Jua kwamba Mungu hakuhesabu makosa yako yote.