Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 51:54-60 Biblia Habari Njema (BHN)

54. “Sikiliza! Kilio kinasikika kutoka Babuloni!Kishindo cha maangamizi makubwakutoka nchi ya Wakaldayo!

55. Maana mimi Mwenyezi-Mungu naiangamiza Babuloni,na kuikomesha kelele yake kubwa.Adui ananguruma kama mawimbi ya maji mengi,sauti ya kishindo chao inaongezeka.

56. Naam, mwangamizi anaijia Babuloni;askari wake wametekwa,pinde zao zimevunjwavunjwa.Mimi Mwenyezi-Mungu ni Mungu mwenye kuadhibu,hakika mimi nitalipiza kisasi kamili.

57. Nitawalewesha wakuu na wenye hekima wake,watawala wake, madiwani na askari wake;watalala usingizi wa milele wasiinuke tena.Nasema mimi mfalme ambaye jina langu ni Mwenyezi-Mungu wa Majeshi.

58. “Mimi Mwenyezi-Mungu wa Majeshi nasema:Ukuta mpana wa Babuloniutabomolewa mpaka chini,na malango yake marefuyatateketezwa kwa moto.Watu wanafanya juhudi za bure,mataifa yanajichosha maana mwisho wao ni motoni!”

59. Mnamo mwaka wa nne wa utawala wake, mfalme Sedekia alikwenda Babuloni pamoja na ofisa wa askari wake aitwaye Seraya mwana wa Neria na mjukuu wa Maseya. Kutokana na fursa hiyo mimi Yeremia nilimpa Seraya ujumbe.

60. Nilikuwa nimeandika kitabuni maafa yote niliyotangaza juu ya Babuloni na pia maneno mengine kuhusu Babuloni.

Kusoma sura kamili Yeremia 51