Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 51:42-59 Biblia Habari Njema (BHN)

42. Bahari imefurika juu ya Babuloni,Babuloni imefunikwa mawimbi yaliyochafuka.

43. Miji yake imekuwa kinyaa,nchi ya ukavu na jangwa,nchi isiyokaliwa na mtu yeyote,wala kupitika na binadamu yeyote.

44. Nitamwadhibu mungu Beli huko Babuloni,nitamfanya akitoe alichokimeza.Mataifa hayatamiminika tena kumwendea.Ukuta wa Babuloni umebomoka.

45. “Tokeni humo enyi watu wangu!Kila mtu na ayasalimishe maisha yake,kutoka hasira kali ya Mwenyezi-Mungu.

46. Msife moyo wala msiwe na hofu,kwa sababu ya uvumi mnaosikia nchini.Mwaka huu kuna uvumi huu,mwaka mwingine uvumi mwingine;uvumi wa ukatili katika nchi,mtawala mmoja dhidi ya mtawala mwingine.

47. Kweli siku zaja,nitakapoadhibu sanamu za Babuloni;nchi yake yote itatiwa aibu,watu wake wote watauawa humohumo.

48. Kisha mbingu, dunia na vyote vilivyomovitaimba kwa furaha kuhusu kuanguka kwa Babuloni,waangamizi watakapofika kutoka kaskazini kuushambulia.Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”

49. Babuloni umesababisha vifo duniani kote;sasa wenyewe utaangamizwa kwa mauaji ya Israeli.

50. “Nyinyi mlinusurika kifo,ondokeni sasa, wala msisitesite!Ingawa mko nchi ya mbali mkumbukeni Mwenyezi-Mungu,ukumbukeni pia mji wa Yerusalemu.

51. Mnasema: ‘Tumeaibishwa na kufadhaishwa;aibu imezifunika nyuso zetu,kwa sababu wageni wameingiakatika sehemu takatifu za nyumba ya Mwenyezi-Mungu.’

52. “Kwa hiyo, wakati unakuja,nasema mimi Mwenyezi-Mungu,ambapo nitaviadhibu vinyago vya Babuloni,na majeruhi watapiga kite katika nchi yake yote.

53. Ingawa Babuloni atapanda mpaka mbinguni,na kuziimarisha ngome zake ndefu,waangamizi watakuja kutoka kwangu kumvamia.2Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.

54. “Sikiliza! Kilio kinasikika kutoka Babuloni!Kishindo cha maangamizi makubwakutoka nchi ya Wakaldayo!

55. Maana mimi Mwenyezi-Mungu naiangamiza Babuloni,na kuikomesha kelele yake kubwa.Adui ananguruma kama mawimbi ya maji mengi,sauti ya kishindo chao inaongezeka.

56. Naam, mwangamizi anaijia Babuloni;askari wake wametekwa,pinde zao zimevunjwavunjwa.Mimi Mwenyezi-Mungu ni Mungu mwenye kuadhibu,hakika mimi nitalipiza kisasi kamili.

57. Nitawalewesha wakuu na wenye hekima wake,watawala wake, madiwani na askari wake;watalala usingizi wa milele wasiinuke tena.Nasema mimi mfalme ambaye jina langu ni Mwenyezi-Mungu wa Majeshi.

58. “Mimi Mwenyezi-Mungu wa Majeshi nasema:Ukuta mpana wa Babuloniutabomolewa mpaka chini,na malango yake marefuyatateketezwa kwa moto.Watu wanafanya juhudi za bure,mataifa yanajichosha maana mwisho wao ni motoni!”

59. Mnamo mwaka wa nne wa utawala wake, mfalme Sedekia alikwenda Babuloni pamoja na ofisa wa askari wake aitwaye Seraya mwana wa Neria na mjukuu wa Maseya. Kutokana na fursa hiyo mimi Yeremia nilimpa Seraya ujumbe.

Kusoma sura kamili Yeremia 51