19. Na watu wenu watakapouliza ‘Kwa nini Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu, ametutendea mambo hayo yote?’ Wewe utawaambia, ‘Nyinyi mlimwacha Mwenyezi-Mungu, mkaitumikia miungu ya kigeni katika nchi yenu. Basi ndivyo mtakavyowatumikia watu wengine katika nchi isiyo yenu.’
20. “Watangazie wazawa wa Yakobo,waambie watu wa Yuda hivi:
21. Sikilizeni enyi wajinga na wapumbavu;watu mlio na macho, lakini hamwoni,mlio na masikio, lakini hamsikii.