10. “Pandeni mpite katika mashamba yake ya mizabibumkaharibu kila kitu bila kumaliza kabisa.Yakateni matawi yake,kwani hayo si yangu mimi Mwenyezi-Mungu.
11. Naam, watu wa Israeli na watu wa Yuda,wamekosa kabisa uaminifu kwangu.Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”
12. Wamesema uongo juu ya Mwenyezi-Munguwamesema: “Hatafanya kitu;hatutapatwa na uovu wowote;hatutashambuliwa wala kuona njaa.
13. Manabii si kitu, ni upepo tu;maana neno lake Mungu halimo ndani yao.”Basi hayo na yawapate wao wenyewe!
14. Mwenyezi-Mungu wa majeshi asema hivi:“Kwa kuwa wao wamesema jambo hilo,sasa nitayafanya maneno niliyokupa wewe Yeremia kuwa moto.Watu hawa watakuwa kuni,na moto huo utawateketeza.
15. “Nami Mwenyezi-Mungu nasema juu yenu enyi Waisraeli:Mimi naleta taifa moja kutoka mbali,lije kuwashambulia.Taifa ambalo halishindiki,taifa ambalo ni la zamani,ambalo lugha yake hamuifahamu,wala hamwezi kuelewa wasemacho.
16. Mishale yao husambaza kifo;wote ni mashujaa wa vita.
17. Watayala mazao yenu na chakula chenu;watawamaliza watoto wenu wa kike na wa kiume.Watachinja makundi yenu ya kondoo na ng'ombe;wataiharibu mizabibu yenu na mitini yenu.Miji yenu ya ngome mnayoitegemea,wataiharibu kwa silaha zao.
18. “Lakini, hata katika siku hizo mimi Mwenyezi-Mungu nasema, sitawaangamiza na kuwamaliza kabisa.
19. Na watu wenu watakapouliza ‘Kwa nini Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu, ametutendea mambo hayo yote?’ Wewe utawaambia, ‘Nyinyi mlimwacha Mwenyezi-Mungu, mkaitumikia miungu ya kigeni katika nchi yenu. Basi ndivyo mtakavyowatumikia watu wengine katika nchi isiyo yenu.’
20. “Watangazie wazawa wa Yakobo,waambie watu wa Yuda hivi: