Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 46:6-11 Biblia Habari Njema (BHN)

6. Walio wepesi kutoroka hawawezi,mashujaa hawawezi kukwepa;huko kaskazini kwenye mto Eufratewamejikwaa na kuanguka.

7. Nani huyo aliye kama mto Nili uliofurikakama mito inayoumuka mawimbi?

8. Misri ni kama mto Nili uliofurikakama mito inayoumuka mawimbiIlisema: “Nitajaa, nitaifunika nchi,nitaiharibu miji na wakazi wake.

9. Songeni mbele, enyi farasi,shambulieni enyi magari ya farasi.Mashujaa wasonge mbele:Watu wa Kushi na Puti washikao ngao,watu wa Ludi, stadi wa kutumia pinde.”

10. Siku hiyo ni siku ya Mwenyezi-Mungu wa majeshi,ni siku ya kulipiza kisasi;naam, siku ya kuwaadhibu maadui zake.Upanga utawamaliza hao na kutosheka,utainywa damu yao na kushiba.Maana Mwenyezi-Mungu wa majeshi anayo kafarahuko kaskazini karibu na mto Eufrate.

11. Pandeni Gileadi, enyi watu wa Misri,mkachukue dawa ya marhamu.Mmetumia dawa nyingi bure;hakuna kitakachowaponya nyinyi.

Kusoma sura kamili Yeremia 46