Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 46:5-18 Biblia Habari Njema (BHN)

5. Lakini mbona nawaona wametishwa?Wamerudi nyuma.Mashujaa wao wamepigwa,wamekimbia mbio,bila hata kugeuka nyuma.Kitisho kila upande.Mwenyezi-Mungu amesema.

6. Walio wepesi kutoroka hawawezi,mashujaa hawawezi kukwepa;huko kaskazini kwenye mto Eufratewamejikwaa na kuanguka.

7. Nani huyo aliye kama mto Nili uliofurikakama mito inayoumuka mawimbi?

8. Misri ni kama mto Nili uliofurikakama mito inayoumuka mawimbiIlisema: “Nitajaa, nitaifunika nchi,nitaiharibu miji na wakazi wake.

9. Songeni mbele, enyi farasi,shambulieni enyi magari ya farasi.Mashujaa wasonge mbele:Watu wa Kushi na Puti washikao ngao,watu wa Ludi, stadi wa kutumia pinde.”

10. Siku hiyo ni siku ya Mwenyezi-Mungu wa majeshi,ni siku ya kulipiza kisasi;naam, siku ya kuwaadhibu maadui zake.Upanga utawamaliza hao na kutosheka,utainywa damu yao na kushiba.Maana Mwenyezi-Mungu wa majeshi anayo kafarahuko kaskazini karibu na mto Eufrate.

11. Pandeni Gileadi, enyi watu wa Misri,mkachukue dawa ya marhamu.Mmetumia dawa nyingi bure;hakuna kitakachowaponya nyinyi.

12. Mataifa yamesikia aibu yenu,kilio chenu kimeenea duniani kote;mashujaa wamegongana wenyewe kwa wenyewe,wote pamoja wameanguka.

13. Neno ambalo Mwenyezi-Mungu alimwambia Yeremia wakati alipofika Nebukadneza mfalme wa Babuloni kuishambulia nchi ya Misri:

14. “Tangaza nchini Misri,piga mbiu huko Migdoli,tangaza huko Memfisi na Tahpanesi.Waambie: ‘Kaeni tayari kabisamaana upanga utawaangamiza kila mahali.’

15. Kwa nini shujaa wako amekimbia?Mbona fahali wako hakuweza kustahimili?Kwa sababu mimi Mwenyezi-Mungu nilimwangusha chini!

16. Wengi walijikwaa, wakaanguka,kisha wakaambiana wao kwa wao:‘Simameni, tuwaendee watu wetu,turudi katika nchi yetu,tuukimbie upanga wa adui.’

17. “Naye Farao, mfalme wa Misri, mpangeni jina hili:‘Kishindo kitupu!’

18. Mimi naapa kwa uhai wangunasema mimi mfalme niitwaye Mwenyezi-Mungu wa majeshi,kweli adui anakuja kuwashambulieni:Ni hakika kama Tabori ulivyo mlimakama mlima Karmeli uonekanavyo kutoka baharini.

Kusoma sura kamili Yeremia 46