Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 4:29-31 Biblia Habari Njema (BHN)

29. Watakaposikika wapandafarasi na wapiga mishale,kila mmoja atatimua mbio.Baadhi yao watakimbilia msituni,wengine watapanda majabali.Kila mji utaachwa tupu;hakuna mtu atakayekaa ndani.

30. Nawe Yerusalemu uliyeachwa tupu,unavalia nini mavazi mekundu?Ya nini kujipamba kwa dhahabu,na kujipaka wanja machoni?Unajirembesha bure!Wapenzi wako wanakudharau sana;wanachotafuta ni kukuua.

31. Nilisikia sauti kama ya mwanamke anayejifungua,yowe kama anayejifungua mtoto wa kwanza.Ilikuwa sauti ya Yerusalemu akitweta,na kuinyosha mikono yake akisema,‘Ole wangu!Wanakuja kuniua!’”

Kusoma sura kamili Yeremia 4