29. Watakaposikika wapandafarasi na wapiga mishale,kila mmoja atatimua mbio.Baadhi yao watakimbilia msituni,wengine watapanda majabali.Kila mji utaachwa tupu;hakuna mtu atakayekaa ndani.
30. Nawe Yerusalemu uliyeachwa tupu,unavalia nini mavazi mekundu?Ya nini kujipamba kwa dhahabu,na kujipaka wanja machoni?Unajirembesha bure!Wapenzi wako wanakudharau sana;wanachotafuta ni kukuua.
31. Nilisikia sauti kama ya mwanamke anayejifungua,yowe kama anayejifungua mtoto wa kwanza.Ilikuwa sauti ya Yerusalemu akitweta,na kuinyosha mikono yake akisema,‘Ole wangu!Wanakuja kuniua!’”